Allah Mwenye kusikia Mwenye kuona

Allah Mwenye kusikia Mwenye kuona

Allah Mwenye kusikia Mwenye kuoNa

Hakika yeye Allah Ni Mwenye kusikia Mwenye kuoNa:

Ewe Mwenye kusikia! Sikiza dua zetu Na utuitikie maombi yetu; kWasababu wewe uNaoNa matendo yetu Na mapungufu yetu Na haja zetu kWako.

“Allah Mwenye kusikia”… ANasikia sauti zote zilizo dhaifu Na zilizo Na nguvu, haimshughulishi sauti mpaka impite sauti nyengine, Wala mwenye kuomba Kwa mwengine.

“Allah Mwenye kuoNa”… ANaoNa kila kitu hata Kama kitakuWa kidogo vipi au kikubWa vipi au kijifiche katika usiku au mchaNa.

“Mwenye kusikia”… ANasikia maneno hata Kama lugha zitahitlafiaNa Na kutafautiaNa maombi pia.

“Mwenye kusikia Mwenye kuoNa” … ANasikia maneno yako, basi jihesabu Nafsi yako, Na aNasikia maombi yako basi mlimlie Mola Wako, Na aNaoNa vitendo vyako hakuNa kitu kiNachofichika , basi fanya wema kWaNi Allah aNaWapenda Watu wema.

“Mwenye kuoNa”… Mwenye kumuoNa sisimizi mweusi katika usiku WA Giza juu ya jabali jeusi, aNaoNa yaliyoko chiNi ya ardhi ya Saba, Kama vile aNavyooNa juu ya mbingu ya Saba.

“Mwenye kusikia Mwenye kuoNa”… Hakifichiki kitu kWake, Wala hakipotei kidogo Wala kikubWa.

Hakika yeye Allah Ni Mwenye kusikia Mwenye kuoNa…



Tags: